Monday, October 8, 2012

"MWENYE MAONO HUWA SELECTIVE, HAOI/HAOLEWI KWASABABU TU KUNA MTU AMEONYESHA NIA"

Haijalishi Una Njaa Ya Kuolewa/Kuoa Kiasi Gani, Kama Umebeba Maono Ya Kimungu Ndani Yako, Chunga Sana Maamuzi Yako Juu Ya Nani Unaunganisha Naye Maisha Yako Kama Mume Au Mke.Kumbuka Si Kila Anayekuja Kwako Kwa Lengo La Kukuoa/Kuoa Anamsukumo Wa Kimungu Ndani Yake.Wengine Wanakuja Kwako Kwa Hila, Na Shetani Anataka Kuwatumia Kuua Maono Mungu Aliyoweka Ndani Yako.Laiti Samsoni Angelijua Hila Iliyokuwa Ndani Ya Moyo Wa Delila Dhidi Ya Kile Mungu Alichoweka Ndani Yake, Kamwe Asinge Thubutu Kujenga Hata Ukaribu Naye.

Hupaswi Kulisha Njaa Yako,Lisha Maono Mungu Aliyoweka Ndani Yako.Wengi Wamejikuta Wakilisha Njaa Zao Za Kutaka Kuwa Na Wenza Na Si Maono Yao, Na Hivyo Kujikuta Wakioa/Kuolewa Na Watu Ambao Ni Waua...
Maono (Vison Killer). Haijalishi Umengoja Kwa Muda Mrefu Kiasi Gani Au Umri Wako Unakimbia Kiasi Gani, Chunga Sana Maamuzi Yako Usije Ukakuta Unalisha Njaa Yako Na Kuunganisha Maisha Yako Na Mtu Yeyote Tu Maadamu Ametokea.

Maono Mungu Aliyoweka Ndani Yako Yana Thamani Kuliko Unavyofikiri.Kumbuka Njaa Haichagui,Njaa Ilimfanya Esau Asione Thamani Ya Uzaliwa Wake Wa Kwanza Na Hivyo Kupoteza Baraka Zote Zailizobebwa Ndani Ya Ile Nafasi.Njaa Yako Ya Kuolewa/Kuoa Isije Kufanya Ukapoteza Maono Yenye Thamani Ambayo Mungu Ameyaachilia Moyoni Mwako. Kaa Na Mungu Vizuri Yeye Anamjua Mwenza Sahihi Kwa Ajili Yako,Tena Atakaye Kusaidia Kukamilisha Maono Yaliyo Ndani Yako.Shaloom!

Monday, September 3, 2012

‘’UNAHITAJI UFUNUO MPYA UTAKAOACHILIA MBINU MPYA ILI UZIKABILI CHANGAMOTO MPYA KATIKA KILA UTUKUFU MPYA MUNGU ANAOKUPELEKA‘’

Kufaulu Kwako Katika Kuzikabili Changamoto Za Jana Hakukupi Garantii Ya Kwamba Utafaulu Kwenye Kukabiliana Na Cha...
ngamoto Unazokutana Nazo Leo Au Utakazo Kutana Nazo Kesho.Ndio Maana Usijaribu Kuingia Katika Kiwango Kipya Kwenye Eneo Lolote La Maisha Yako Ukiwa Na Mbinu Za Zamani Pekee Na Ukategemea Kufaulu Vizuri Katika Kukabiliana Na Changamoto Utakazokumbana Nazo Kwenye Hicho Kiwango Mungu Atakacho Kupeleka.

Kumbuka Kadiri Mungu Anavyokutoa Kwenye Kiwango Kimoja Cha Utukufu Kwenda Kwenye Utukufu Mwingine Ndivyo Adui Anavyozidi Kujipanga Na Kuongeza Jitihada Katika Kukufuatilia Na Kukupinga.Upinzani Uliokutana Nao Kwenye Utukufu Mungu Aliokupitisha Jana Nitofauti
Kabisa Na Upinzani Utakao Kutana Nao Kwenye Utukufu Mungu Anaokupitisha Leo Au Kesho.Ndio Maana Mbinu Ulizozitumia Kukabiliana Na Changamoto Za Jana Zinaweza Zisiwe Bora Leo Kama Itaibuka Changamoto Mpya Isiyofanana Na Ile Uliyokabiliana Nayo Jana.

Daudi Alijua Hili Na Ndio Maana Alikataa Mavazi Na Dhana Za Kijeshi Alizotaka Kuvalishwa Na Mfalme Sauli Wakati Anajiandaa Kumkabili Goliath. Daudi Alijua Mapema Kwamba Hivyo Vitu Vya Sauli Ni Mbinu Za Zamani Na Hazina Msaada Vinginevyo Jeshi La Israel Lisingeshindwa Kumkabili Goliathi Hapo Kabla.Alijua Anahitaji Ufunuo Mpya Toka Kwa Mungu Na Si Ule Wa Zamani Wa Mfalme Sauli.Ni Ufunuo Mpya Ulioachilia Mbinu Mpya Na Ndizo Zilizomvusha Daudi Dhidi Ya Goliathi.

Maombi Yangu Na Dua Yangu,Ni Mungu Akakupe Ufunuo Mpya Utakao Achilia Mbinu Mpya Za Kukabiliana Na Changamoto Mpya Utakazokutana Nazo Kadiri Anavyozidi Kukupeleka Kwenye Utukufu Mpya Kila Inapoitwa Leo.Shaloom!!

Sunday, July 29, 2012

“UMEKUJA DUNIANI KWASABABU UNAHITAJIKA”
Mshukuru Mungu Kwasababu Wakati Unazaliwa Changamoto Ndani Ya Dunia Hii Zilikuwa Hazijaisha, Vingenenyo Ungekuwa Hauna Kazi Ya Kufanya Hapa Duniani.Tena Usijeukafikiri Ni Bahati Mbaya Kwamba Umezaliw...a Ndani Ya Nchi/Familia Yenye Changamoto Chungu Mzima Na Ukaanza Kujichukia Na Kulaani. Nataka Ufahamu Hili Mtu Wa Mungu, “Wewe Ni Original (Sio Fotokopi) Na Umekuja Duniani Kwasababu Unahitajika”

Mungu Amekuleta Duniani Kama “Spana” Maalumu Kwa Ajili Ya Kukutumia Kufungulia Nati (Changamoto) Zote Zilizogoma Kufunguka Katika Mazingira Yako. Amekudesign Katika Ufanisi Wa Kipekee Kiasi Kwamba Hakuna Nati Aliyoikusudia Aifungue Kwakukutumia Wewe Ambayo Itakayogoma Kufunguka Ikiwa Utakubali Akutumie. Kuna Nati (Changamoto) Chungu Mzima Hazija Funguka Mpaka Leo Hii Katika Familia Yako,Katika Nchi Yako Kwasababu Tu Umekataa Kukaa Kwenye Nafasi Yako Ili Mungu Akutumie Kuzifungua Nati (Changamoto) Hizo.

Ndio Maana Nataka Nikukumbushe Hili Leo, “Umekuja Duniani Kwasababu Unahitajika”.Mungu Anakuhitaji,Jamii Inakuitaji,Kanisa Linakuhitaji,Familia Yako Inakuitaji.Usipo Simama Kwenye Nafsi Yako Sawasawa,Kuna Nati(Changamoto) Humu Duniani Hazita Funguka Maana Wewe Ndiye Uliyedesigniwa Na Mungu Akutumie Kushughulikia Hizo Nati(Changamoto).Simama Katika Nafasi Yako Mtu Wa Mungu Maana Saa Ya Wokovu Ni Sasa.Shaloom!
“KUOKOKA PASIPO KUTEMBEA KWENYE KUSUDI LA MUNGU HAKUMTISHI SHETANI”

Shetani Haogopi Watu Waliookoka, Anaogopa Watu Waliookoka Na Wanaotembea Kwenye Makusudi Ya Mungu. Vita Ya Shetani Si Kukuzuia Wewe Kwenda Mbinguni Tu, Bali Ni Pamoja Na K...uhakikisha Kwamba Makusudi Ya Mungu Humu Duniani Hayafanikiwi.Na Ndio Maana Wakati Mwingine Anaweza Asilete Upinzani Kwenye Kuokoka Kwako.Akakuacha Uokoke Bila Upinzani Wowote, Lakini Mara Tu Baada Ya Kuokoka Akakupiga Vita Na Kukutengenezea Mazingira Ya Kukufanya Uishi Nje Ya Kusudi Mungu Alilonalo Juu Ya Maisha Yako.

Kwenda Mbingu Wakati Umetumia Maisha Yako Nje Ya Makusudi Ya Mungu Ni Kuutia Hasara Ufalme Wa Mbinguni.Mungu Amekuokoa Sio Tu Uende Mbinguni, Bali Pia Uishi Maisha Ya Ushindi Huku Ukilitumikia Kusudi Lake Hapa Duniani.Ndio Maana Kuna Maelfu Ya Watu Wameokoka Na Shetani Amekua Akiwavuruga Kila Eneo Kwasababu Hawatembei Kwenye Kusudi Mungu Alilowaitia. Kamwe Usitegemee Masaada Wa Mungu Nje Ya Kusudi. Na Ukikaa Nje Ya Kusudi Ujue Unampa Shetani Uhalali Wa Kukuvuruga, Na Mungu Hawezi Kukutetea Nje Ya Kusudi.Ndio Maana Ni Muhimu Ujue Hili, Ukiokoka Na Hautembei Kwenye Makusudi Ya Mungu Jua Hauna Madhara Kwa Shetani.Shalooom!

Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa;<< Yeremia 1:5a>>

USIJARIBU KULEGEZA MSULI WAKO WA IMANI KAMA UNAJUA HUJAIINGIA KANANI YAKO

Ni Muhimu Kukumbuka Hili, ‘‘Unapo Piga Hatua Moja Mbele Kwenye Eneo Lolote La Maisha Yako Iwe La Kiroho,Kibiashara,Kielimu,Au Kwenye Lolote Lile Linalombariki Mungu....Kamwe Usije Ukajisahau Na Kulegeza Msuli Wako Wa Imani.’’ Shetani Hatokubali Kamwe Uiendee Hatima Yako Na Hivyo Atakufuatilia Kwa Namna Yeyote Ile Ili Akurudishe Nyuma(Utumwani).

Na Moja Ya Kitu Atakacho Pambana Kukiharibu Ni Imani Iliyojengeka Ndani Yako.Anajua Akibomoa Imani Iliyojengeka Ndani Yako, Utaanza Kuangalia Ukubwa Wa Bahari Iliyo mbele Yako,Utaanza Kulihofu Jeshi Linalo Kufuatailia Nyuma Ili Kukurudisha Misri.Tena Utasahau Ukuu Na Uaminifu Wa Mungu Aliyekufikisha Mahali Ulipo. Na Mwisho Atakurejesha Nyuma (Utumwani) Kirahisi Kabisa.

Kadiri Unapotoka Utukufu Kwenda Utukufu Ndivyo Adui Anavyozidi Kujipanga Na Kuongeza Jitihada Katika Kukufuatilia.Uimara Wa Imani Yako Ndio Utakao Kusaidia Kupata Msaada Wa Mungu Pale Unapokutana Na Upinzani. Kumbuka,Mungu Hakukutoa Misri Ili Urejee Tena Huko,Wala Hakukutoa Misri Ili Uje Kuangamia Njiani. Na Ndio Maana Kama Unajua Umepiga Hatua Fulani Lakini Haujaifikia Kanani Yako Usije Ukajaribu Kulegeza Msuli Wako Wa Imani.Kumbuka Bado Utahitaji Msaada Wa Mungu Ili Uifikie Kanani Yako, Na Pasipo Imani Iliyojengwa Sawasawa Itakuwa Ni Vigumu Kupokea Msaada Huo Na Hata Kuzikabili Changamoto Zitakazokujia Mbele Yako.Shaloom!


‘Zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu’.<<Waefeso 6:15 >>
See More

“WEWE NI ORIGINO USIJARIBU KUISHI KAMA KOPI”

Umewahi Kufikiri Kwanini Tangu Misingi Ya Dunia Hii Ilipowekwa Mpaka Dakika Hii Unaposoma Post Hii ,na Hata Miaka Itakayokuja Huko Mbele,Hajawahi Kuwepo,Hayupo Na Hatakuwepo Mtu Mwenye Kufanana ...na Wewe Kwa 100%?

Kuzungumza Kwako, Kufikiri Kwako,Kutenda Kwako,Kuamua Kwako, Kwote ni Kwa Tofauti na Kwa kipekee Kabisa.Hata Alama Za Vidole Gumba Vyako Havifanani na Vya Mtu Yeyote Yule Hapa Duniani.Unadhani Ilitokea Tu Kama Bahati Mungu Aamue Kutumia Mda Wake,Ubunifu na Kila Alichotumia Ili Tu Akutengeneze Kwa Ustadi Mpaka Utoke Original Namna Hii? Ni Wazi Kabisa Mungu Angeweza Kuokoa Muda Wake Na Kuamua Kukufotokopi,Uzaliwe Kama Kopi Kutoka Kwa Wazazi Wako Lakini Hakufanya Hivyo,Akaamua Kukutoa Original Unafikiri Ni Bure Bure Tu?

Sikiliza Mtu Wa Mungu,Kamwe Usijaribu Kuishi Ishi Tu Ilimradi Siku Ziende,Tena Usijaribu Kuishi Kama Mtu Fulani Kwani Ni Hatari Kwa Habari Ya Hatima Yako.Mungu Ameamua Kukutengeneza Original Na Kuwekeza Vitu Hivi Vyote Vya Kipekee Ndani Yako Kwasababu Analo Kusudi La Kipekee Kwa Habari Ya Maisha Yako.Usijaribu Kuishi Kama Kopi,Mungu Haitaji Kopi Yako Anataka Origina Yako Maana Ndiyo Aliyoiandaa Kwa Ajili Ya Kutekeleza Makusudi Yake Hapa Chini Ya Jua.Shaloom!
See More

Thursday, July 5, 2012

“USIJARIBU KUITAMANI KANANI KAMA HAUKOTAYARI KUPAMBANA NA MAJITU (CHANGAMOTO)”

Ni Kweli Kanani Kuna Maziwa Na Asali,Tena Ni Nchi Nzuri Ajabu, Lakini Kuna Majitu (Changamoto) Yanayoishi Humo.Na Hivyo Yeyote Anayetaka Kufurahia Mazuri Hayo Y...a Kanani Ni Lazima Awetayari Kukabiliana Na Majitu(Changamoto) Ndani Ya Hiyo Kanani.Kama Unayaogopa Majitu(Changamoto) Sahau Habari Za Maziwa Na Asali Maana Hutoyapata.

Umewahi Kujiuliza Kwanini Mungu Akuandalie Kanani Yenye Maziwa Na Asali Na Wakati Huo Huo Aruhusu Majitu Yakae Ndani Ya Hiyo Kanani? Kwanini Mungu Asiwaondoe Majitu Hayo (Changamoto Hizo) Kwanza Na Ndipo Akuruhusu Uimiliki Kanani Hiyo? Hii Ni Siri Ya Ajabu Mtu Wa Mungu Na Unapaswa Ufahamu. “Katikati Ya Majitu (Changamoto) Kuna Maziwa Na Asali Na Hakuna Jinsi Ya Kuyafurahia Mazuri Hayo Bila Ya Kuyakabiliana na Majitu (Changamoto)”. Na Ukiona Majitu Yanaongezeka Jua Kuna Shehena Ya Maziwa Na Asali Kubwa Kuliko Kawaida Hapo Mahala. Ukijaribu Kuyakimbia Majitu (Changamoto) Jua Ndo Unaikimbia Kanani Yako Na Vyote Vizuri Vilivyomo Ndani Yake.

Pengine Umeikaribia Kanani Yako Mara Nyingi Lakini Kwasababu Umeyaona Majitu (Changamoto) Ukaogopa Na Umeamua Kurudi Nyuma.Ni Heri Ukalijua Hili Mtu Wa Mungu,Hakuna Jinsi Utakayo Weza Kufaidi Mazuri Ya Kanani Kama Hutaki Kuyakabili Majitu(Changamoto) Yaliyomo Ndani Ya Hiyo Kanani.Ukisoma Habari Ya Wapelelezi Kumi Na Wawili Kwenye Kitabu Cha Hesabu Sura 13 & 14, Maandiko Yanatuambia Ni Wale Tu Walionyesha Uhodari Na Utayari Wakutaka Kuyakabili (Majitu) Changamoto (Kalebu Na Yoshua) Ndio Waliopata Kibali Cha Kuiingia Nchi Ya Ahadi(Kanani).
Ukiamua Kuogopa Kuyakabili Majitu Na Kuyaachia Ya Faidi Maziwa Na Asali Ndani Ya Kanani Mungu AliyoKukusudia, Uamuzi Ni Wako.Ukiamua Kuyakabili Majitu Ili Umiliki Na Kuyafurahia Mazuri Ya Kanani Yako.Uamuzi Ni Wako.Chagua Lako!Shaloom!

“Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu” <<Zaburi 23:5a>>